
BISKUTI ZA SIAGI
Maandalizi; dakika 15
Muda wa kupika; dakika 15
Muda jumla; dakika 30
MAHITAJI
➖Kikombe 1 siagi
1/2 kikombe icing sugar
➖Kijiko 1 cha chai vanilla extract
➖Vikombe 2 unga wa ngano
1/4 kijiko cha chai chumvi
MAELEZO
⭕Anza kwa kuwasha oven joto la 175 degrees C ili ipate joto wakati unachanganya unga. Kwenye bakuli kubwa changanya siagi, icing sugar na chumvi mpaka mchanganyiko ulainike vizuri. (unaweza kutumia mashine au bila mashine. Ni rahisi zaidi ukitumia mashine). Ongeza vanilla, changanya kwa dakika kama moja nyingine
⭕Ongeza unga wa ngano. Kanda mpaka uchanganyike vizuri kabisa
⭕Gawanya mchanganyiko wa unga kwa kipimo cha kijiko 1 cha chakula, tengeneza mduara kama vimpira. Panga vizuri kwenye chombo cha kuokea ukitumia karatasi za kuokea.
⭕Hakikisha umeacha nafasi ya kutosha katikati ya kila biskuti.
⭕Kandamiza kila donge la biskuti kwa kutumia cookies stamp, uma, glasi ya maji au kifaa chochote utakachotumia kutengeneza umbo unalotaka
⭕Hakikisha unachovya kifaa cha kutengenezea umbo la biskuti kwenye icing sugar ili kusaidia unga usinate kwenye kifaa na pia umbo litokee vizuri zaidi
⭕Oka kwenye oven iliyopata moto katika joto ya 175 degrees kwa dakika 12-15 au mpaka zianze kupata rangi ya kahawia chini.
⭕ Usishangae zikiwa laini sana wakati unazitoa kwenye oven, ni kawaida zikipoa zinakuwa kawaida
⭕Ipua, acha zipoe kwa dakika 5 kabla ya kuhamishia kwenye waya wa kupozea zipoe kabisa.
Kwa mapishi zaidi ya cookies na biscuits, jipatie kitabu
0 Comments
Welcome to comment