MKATE WA MAYAI ( SPONGE CAKE )
*MAHITAJI*
 Mayai sita
 Sukari nusu kikombe
unga kikombe kimoja
hiliki
 vanilla(si lazima)
zabibu kavu(si lazima)
baking powder kijiko cha chai 1
*MATAYARISHO*
Tayarisha sufuria ya kiasi na uipake mafuta.
Weka mayai, sukari na iliki kwenye bakuli uanze kupiga Kwa mashini(mixer) au mchapio mpaka mayai yafure yaani yazidi yawe mara mbili yake.
Anza kuweka unga kidogo kidogo huku ukikoroga taratibu kisha ufuatie na vanilla.
Weka mchanganyiko wote kwenye sufuria.
Tupia tupia zabibu juu ya mchanganyiko.
Bake mkate wako Kwa moto wa juu na chini kwenye jiko la makaa( hakikisha moto kwenye jiko ni kidogo sana alafu ukifinika ueke makaa ya kutosha juu ya utakachofunikia sufuria, mfuniko
 unaweza ukabake kwa oven kwa Moto wa 250°C takriban nusu saa(itategemea na aina ya oven)
bofya mkate wako Kwa kijiti. Kijiti kikitoka kikavu mkate upo tayari.
NB:
zingatia:
*mkate wa mayai hautiwi siagi, blueband, butter wala mafuta.
Ni ngano tu na mayai
*kipimo kizuri cha mkate cha mayai ni ujazo wa ngano na ujazo wa mayai uwe sawa sawa, yaani kwa mfano unga glass moja basi na mayai yafikie ujazo huo huo wa glass moja.
*wakati wa kupiga mayai inatakiwa usiache ache mkono, upige au kukoroga mpaka yafanye povu; itafanya mkate uvimbe vizuri.
*mkate huu uko soft na mlaini kuliko keki ndio maana ukaitwa sponge cake.
0 Comments: