
BIRIANI YA KUKU WA KIENYEJI
MAHITAJI 😚
BASMAT RICE
RANGI ZA CHAKULA
TOMATO PASTE
NYAMA YA KUKU
NYANYA MAJI
MAZIWA MTINDI
VITUNGUU MAJI
CHUMVI
MAFUTA YA KUPIKIA
VIAZI MVIRINGO
GILIGILANI
ZABIBU KAVU
Kitunguu saumu na tangawizi
Carrot
Hoho
Binzari ya manjano
Binzari nyembamba
Namna ya kutayarisha 🖤
Chukua nyama yako ya kuku ioshe ichemshe weka Kitunguu saumu tangawizi ,limao na iache ichemke mpaka iive
Baada ya kuiva Chukua nyanya maji katakata weka kwenye blender pamoja na GILIGILANI na maziwa mtindi saga kwa pamoja
Chukua Sufuria Weka mafuta ya kutosha Kisha Chukua Vitunguu maji ulivyokata vya kutosha kaanga vikiwa Golden brown vitoe weka kwenye sahani
Kwenye mafuta yaleyale kaanga viazi mviringo vyako na vikiwa brown vitoe
Chukua Sufuria Weka ile nyama ya kuku na weka ule mchanganyiko wa nyanya na mtindi Vitunguu maji ,mafuta ya kupikia ,Chumvi ,Kitunguu saumu na tangawizi na mafuta kiasi acha vichemkie
Vikichemka weka tomato paste, binzari ya manjano na binzari nyembamba changanya Kisha weka Hoho na carrot acha vichemkie Kisha Weka viazi mviringo acha mchuzu uchemke mpka uwe mzito
Chukua Sufuria Weka maji kiasi yakichemka weka Chumvi mafuta ya kupikia na mchele wako koroga kidogo kidogo mpka maji yakauke
Yakikauka Chukua rangi zako kulingana na rangi unazopenda mwagia kwa juu na utatupia zabibu kavu Kisha palilia wali wako au funika kwa mfuko laini baada ya hapo utageuza na utachanganya na rangi zako uchanganyikane vizuri pakua chakula chako rosti la nyama weka kwa juu na biriani lako lipo tayari kuliwa na pilipili
Enjoy 😋😋😋😋😋😋
Jifunze kupika mapishi hapa mapishiclub.Blogspot.Com
0 Comments
Welcome to comment