Welcome mapishiclub.Blogspot.Com
JINSI YA KUPIKA PILAU LA NYAMA
orodha ya viungo
Mchele kilo1 ¼
Nyama kilo ½
Mafuta yakupikia lita ¼
Njegere kilo ½
Giligilani pakti ndogo 1
Mdalasini ya unga packti ndogo 2
Jira packti ndogo 2
Chumvi packti ndogo 1
Vitunguu-maji kubwa 3
Vitunguu-saumu kubwa 1
Hatua ya kutayarisha viungo
Ukisha andaa vitu vyote hivi tunaanza kuandaa chakula chetu cha Leo
Anza kumenya vitunguu saumu
Katakata vitunguu maji
Chambua girigilan
Kata kata nyama
Chukua vitunguu swaumu, girigilan, jira viweke kwenye kiuri na utwange vizuri hadi vilainike
Hatua na maelekezo ya kupika
Chukua sufuria yako bandika jikoni weka mafuta
Weka vitunguu maji jikoni
Kaanga hadi viwe na ranging ya kahawia
Weka nyama anza kuikaanga
Endelea kugeuza nyama yako ikaange vizuri hadi iive
Chukua mchanganyiko wa vitunguu swaumu, girigilan, jira ulio twanga viweke na endelea kukaanga
Chukua mdalasin weka koroga vizuri
Weka chumvi geuza
Weka njegere zako geuza vizuri ichanganyike
Weka maji acha ichemke kwa dakika tano
Weka mchele geuza vizuri taraaraatibu
Funika na uweka moto mdogo wakuivisha chakula taratibu kwa dakika kumi
Funua chakula chako geuza hapo kitakua pilau iliyo tayari kwa kula
Hitimisho na Mawasiliano ya Mwandishi
Kwa kuhitimisha napenda kusema tu kwamba upishi wa pilau uko wa aina nyingi na hata ndani ya aina moja bado mapishi yanaweza kutofautiana sana na inategemea Zaidi ubunifu wa mpisha kuweza kupindisha pindisha baadhi ya taratibu ili kuweza kupata chakula kizuri, kitamu na kinacho walaji.
Mfano tu kwenye pilau ya nyama unaweza weka nyama nyingi, kawaida au chache, unaweza kubadilisha rangi ikawa kahawia au njano nk
je una maoni usisite kituandikia jjumbe yako katika ukurasa wetu
by Director13
0 Comments
Welcome to comment